1 Corinthians 6:1-6

Kushtakiana Miongoni Mwa Waumini

1 aKama mtu yeyote wa kwenu ana ugomvi na mwenzake, anathubutuje kuupeleka kwa wasiomcha Mungu ili kuamuliwa badala ya kuupeleka kwa watakatifu? 2 bJe, hamjui kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Nanyi kama mtauhukumu ulimwengu, je, hamwezi kuamua mambo madogo madogo? 3 cHamjui kwamba tutawahukumu malaika? Je, si zaidi mambo ya maisha haya? 4 dKwa hiyo kama kuna ugomvi miongoni mwenu kuhusu mambo kama haya, chagueni kuwa waamuzi, watu ambao wanaonekana hata sio wa heshima katika kanisa. 5 eNasema hivi ili mwone aibu. Je, inawezekana kuwa miongoni mwenu hakuna mtu mwenye hekima ya kutosha kuamua ugomvi kati ya waaminio? 6 fBadala yake ndugu mmoja anampeleka mwenzake mahakamani, tena mbele ya watu wasioamini!

Copyright information for SwhKC